DJ BOSTON-ON BEAT U KNOW WAT IT IS!!!

Friday, December 20, 2013

Izzo Bizness Kupiga Show New Years Eve Home …

izzo 

Kila mtu hupenda kumalizia mwaka nyumbani, kama ilivyo kwa msanii huyu mahiri wa kizazi kipya rapper Izzo Bizness … anatarajia kuwapa zawadi kubwa watu wake wa nyumbani alipozaliwa na kukulia mwisho wa mwaka huu. Rapper huyu mkali imeripotiwa kuwa siku ya tarehe 31/12/2013 kama wenzetu wazungu waitavyo New Years Eve, basi rapper huyu atapiga bonge la shoo jijini Mbeya kwa ajili ya kuuaga mwaka wa 2013 ambapo umekuwa mwaka mzuri kwa msanii huyu katika industry ya music na kuukaribisha mwaka mpya wa 2014.
Shoo hiyo ambayo rapper huyu ataperform itakwenda kwa jina la Home Sweet Home, litakalokuwa likifanyika katika Club ya Babz jijini Mbeya.

No comments: