DJ BOSTON-ON BEAT U KNOW WAT IT IS!!!

Sunday, August 11, 2013

RAY C! MUNGU ANATAKA KUKUTUMIA!

Mungu ametumia mkono wa wahalifu kukuteua, na akatumia mkono wa Mhe. Rais Kikwete kuidhinisha uteuzi wake na sasa taifa linasubiri utendaji kazi. Ni kwa njia yako wengi watapona maana vita hii ni ngumu sana kupigwa kwa mtutu wa bunduki na makucha ya Serikali kama ambavyo watu wengi wanadhani. Kwani Serikali zenye nguvu kubwa za kisayansi, kijasusi na kijeshi na sheria ngumu ngumu kama vile Marekani, China, Uingereza nk zenyewe zimeshindwa.
Ushauri wangu mkuu kwako Mpendwa Ray C. Ni wakati Muafaka sasa kwako kuanzisha asasi (NGO) kubwa isiyo ya kiserikali kwa ajili ya kupambana na madawa ya kulevya, asasi ambayo uwe na majukumua makubwa matatu (1) Kuhakikisha waathirika wanapata matibabu na kuacha madawa ya kulevya (2) kutoa Elimu kubwa kwa jamii kupitia vyombo vya habari, mashuleni na vyuoni na katika vikundi vya michezo nk (3) Kupambana na wauza madawa ya kulevya Kisaikolojia kwa kuendesha kampeni ya Elimu ya Kifikra itakayowashawishi kuacha wenyewe biashara hiyo.
 


 
Kwa kupitia asasi (NGO) hiyo namshauri Rais Dr. Jakaya Kikwete aoneshe Huruma na Uzazi kwa vijana na Watanzania wote kama alivyofanya kwa Ray C kwa kusaidia NGO kupata uwezo wa kutekeleza majukumu yake. Ni matumaini yangu kwa msukumo wa Rais Kikwete na umuhimu wake Asasi hiyo itapata wafadhili wakubwa na kufanikisha malengo yake, kama alivyofanikisha ufadhili katika Timu ya Taifa na mambo mengine kadha wa kadha..
 

No comments: