DJ BOSTON-ON BEAT U KNOW WAT IT IS!!!

Thursday, October 31, 2013

Ndoa yamshinda Bob Jr.


 
Msanii Bob Junior ambaye aliingia katika maisha ya ndoa pamoja na kujipatia baraka ya mtoto wa kiume, ameweka wazi kuwa kwa sasa hayupo tena pamoja na mkewe na wametengana, ingawa hakutaka kusema wazi sababu hasa ya kutengana na mkewe huyo.

Bob Junior ametaja wivu kama moja ya sababu zilizofanya ndoa yake kuvunjika na kwamba alikuwa na wakati mgumu sana kumuonyesha mke wake kuwa yeye ni muaminifu kutokana na kuwa star na kupendwa na mashabiki wengi wa Kike.

Wakati huo huo kwa upande mwingine, Bob Junior pia kwa sasa ameachia ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina “Bashasha” akiwa amemshirikisha msanii wa kike anayekuja juu Vanessa Mdee, amewataka mashabiki kuipokea vizuri kazi hii mpya ambayo ina ujumbe mzito wa kimapenzi.

No comments: