DJ BOSTON-ON BEAT U KNOW WAT IT IS!!!

Friday, November 8, 2013

Kus Ma aonyesha ukomavu


 
Rapa kutoka Kenya ambaye umaarufu wake mkubwa uliibuka akiwa na kundi la Camp Mulla, Kus Ma ameendelea kuonyesha uwezo na utaalam mkubwa kimuziki, na hii ni baada ya kuonekana akipiga ngoma kwa umahiri mkubwa katika muziki wa live ndani ya tamasha na Naija Nite hivi karibuni.

Kus Ma ambaye ni mtayarishaji muziki mzuri pia, licha ya umri wake mdogo, amewashangaza wengi waliokuwa hawafahamu kipaji chake hiki cha kupiga muziki live, na hii ni hasa kutokana na kuzoeleka kwa swala kuwa wasanii na wanamuziki wengi wa sasa wamebobea katika muziki wa kidijitali tu.

Kus pamoja na Tiri ambao mbali na kufanya muziki pia ni wapenzi, wameendelea kuendeleza harakati zao za muziki kwa karibu wakiwa pamoja kwa muda sasa, na hii ni baada memba wengine wa kundi la Camp Mulla kuonekana kuwa bize na shughuli zao za binafsi.

No comments: