DJ BOSTON-ON BEAT U KNOW WAT IT IS!!!

Sunday, November 10, 2013

SAID MKUKILA KUMFUNIKA YAKUTI KATIKA SCRIPT?


Said Mkukila




UKIONGELEA asilimia kubwa ya filmu kubwa na nyingi Swahiliwood ukiuliza nani kaandika basi utaambiwa ni mwandishi mahiri wa mswada Bongo ni Ali Yakuti, halina ubishi yeye ndio mwandishi anayetesa hivi sasa kwa kuwa na filamu nyingi zilizoandikwa na yeye, lakini ukiongelea waandishi wanaokuja kwa kasi basi jina la Said Mkukila naye anayesikika kufuata nyayo za Yakuti.

 Said Mkukila
Mkukila anasema kuwa alianza kuandika script baada ya kugundua kuwa waandishi ni wachache lakini kuna wakati ambao anahisi hakuna utofauti au ladha nyingine katika tasnia ya filam jambo linalomfanya achukue muda wake kwa kusoma taaluma ya uandishi wa Muswada na kufanya kazi ambayo ameichagua kwa sasa.
“Kuna watu wananifananisha na waandishi wakubwa waliofanikiwa katika tasnia ya filamu lakini mimi sijifananishi na mtu mwingine kwani kila mtu ana wakati wake na hata mfumo wa uandishi pia unaweza kutofautina kulingana na mapokeo ya stori yenyewe,”anasema Mkukila.
Mwandishi huyo ambaye anaonyesha uchu wa kujifunza na kuwa mwandishi wa kimataifa siku zijazo na kuwa mkombozi wa tasnia ya filamu Bongo, Mkukila hadi sasa amendikia script filamu kama Mbegu, Kigodoro akishirikiana na Omary Clayton, Machozi na Wazanga yangu ambazo zinafanya vizuri sokoni.

No comments: