Ukisema
kwamba Tanzania hakuna “familia za wanamuziki” utakuwa unakosea kwani
jibu ni kwamba zipo. Mojawapo miongoni mwa familia hizo ni ile ya kina
Bushoke. Pichani ni mwanamuziki ambaye hujulikana kwa jina la Bushoke
ambaye ni mtoto wa Max Bushoke, mwanamuziki mkongwe wa Tanzania ambaye
siku hizi anafanya kazi ya utangazaji nchini Afrika Kusini. Max Bushoke
aliwahi kutamba sana nchini Tanzania alipokuwa na bendi kama vile Bima
Lee Orchestra na nyinginezo. Vibao kama Mesenja Kaleta Balaa ni mojawapo ya vibao ambavyo Max hukumbukwa navyo sana.
Kwa
upande wa Bushoke(Junior) kibao ambacho alitamba nacho sana na ambacho
pengine ndio “kilichomtoa” rasmi ni kile kiitwacho Barua. Unaweza
kukisikiliza kwa kubonyeza hapa.Kuna
habari ambazo bado hatujaweza kuzithibitisha zinazosema kwamba
Bushoke(Junior) naye ametimkia Afrika Kusini aliko baba yake ili
kuendeleza shughuli zake za muziki.

No comments:
Post a Comment