DJ BOSTON-ON BEAT U KNOW WAT IT IS!!!

Friday, September 13, 2013

Navio, Keith kuwashangaza watu



Ile kolabo ya mwaka inayomhusisha msanii wa Uganda, Navio pamoja na msanii wa kimataifa Keith Sweat tayari imeshaanza kuwa gumzo mtaani hasa kutokana na uwezo na uzoefu na muunganiko wa wasanii hawea wawili ambao wana heshima za kipekee katika aina za muziki wanaoufanya.
 
Kolabo hii inakwenda kwa jina On and On na imefanyika huko Atlanta Marekani katika studio binafsi ya msanii Keith Sweat, na habari mpya kutokana na mpango huu ni kuwa, mipango ya video ya kazi hii tayari imeanza kufanyika ambapo hivi karibuni Navio anatarajia kurudi Atlanta kwaajili ya kumalizia kazi hii.
 
Wimbo huyu umetajwa pia kushughulikiwa na wataalamu wa kufanya mastering ambao ni wa kimataifa zaidi ili kuleta ladha ambayo itathibitisha ushiriki wa wakongwe na wasanii wanaoweza na kujua kile wanachokifanya.

No comments: