DJ BOSTON-ON BEAT U KNOW WAT IT IS!!!

Friday, November 8, 2013

AY (@AyTanzania) Apanda Chati Kwenye Ligi Ya Twitter… #TwitterLeague #Choamva

#CHOAMVA

 
Msanii AY ambaye anafanya vizuri kuiwakilisha nchi ya Tanzania kwenye tuzo zinazotarajia kufanyika hivi karibuni za Channel O, amefanikiwa kuwapiku washiriki wengine na kupanda kwenye Top 5 ya #TwitterLeague #Choamva baada ya kuwatupa Radio & Weasel kwenye kinyang’anyiro kinachoendelea ndani ya chati iyo..
AY anakamata namba 4 sasa kwenye ligi hiyo toka nafasi ya 6 siku ya jana, ambapo Radio na Weasel ndiyo wanashikila nafasi hiyo
Endelea kumtaja AY on Twitter pamoja na kuweka hashtag ya #CHOAMVA uongelee chochote kumhusu, ili mwakilishi wetu huyu azidi kupanda chati! Tanzania tunaweza … Na bila kusahau kumpigia kura msanii AY kwa ajili ya kumwezesha kuibuka mshindi katika tuzo ambazo anaziwania Channel O.

No comments: