DJ BOSTON-ON BEAT U KNOW WAT IT IS!!!

Wednesday, November 13, 2013

Benjamin kupiga shule zaidi


 
Msanii mahiri wa muziki hapa Bongo ambaye hivi sasa pia anapiga mishe za kutengeneza video za muziki kati ya nyinginezo, Benjamin Busungu, maarufu kama Benja wa Mambo Jambo ameweka wazi mpango wake wa kuingia shule na kuendelea zaidi maujuzi yake katika maswala ya video production.

Mkali huyu ambaye ametua hivi karibuni akitokea huko Afrika Kusini, akiwa na nia ya dhati ya kutela mapinduzi katika swala zima la kiwango na utaalam wa video za muziki bongo amesema kuwa ataanza kuingia darasani mwezi wa nne mwaka kesho kujinoa zaidi katika maswala ya motion film pamoja na kutengeneza mahusiano na ma-director wa kimataifa wa videos na pia kupata cheti ambacho kitasaidia kukubalika kwa kazi zake za video hata katika vituo vya kimataifa vya televisheni.

Benjamin amesema kuwa katika kipindi hiki pia atatumia nafasi aliyoipata kuwavuta wasanii wa hapa nyumbani na kufanya nao video za kiwango cha kimataifa huko Afrika Kusini na hivyo kujenga heshima ya video na ma-directors wa hapa nyumbani katika swala zima la viwango vya kazi wanazozitengeneza.

No comments: