DJ BOSTON-ON BEAT U KNOW WAT IT IS!!!

Tuesday, November 5, 2013

HALI YA BONGO FLEVA ILIVYO SASA USIKURUPUKE – BEN PAUL.



 
Mashairi yake na mtindo wa uimbaji anaoutumia kwenye ngoma zake unamfanya awe ni mmoja kati ya wasanii wakali zaidi kwa nyakati hizi Tanzania.

Uwezo wake kiuimbaji ndo umemfanya achukue tuzo kila mwaka tangu rasmi kuzitambulisha ngoma zake redioni. Mpaka sasa ameshagonga ngoma kali nyingi kama vile Nikikupata, Pete n.k na hivi karibuni anatesa na ngoma yake ya Jikubali.
“Najiamini sana kwamba nina uwezo na namshukuru Mungu hata wasanii wenzangu wengi wananikubali sana na kunishauri mengi lakini hii hali hainifanyi mimi kufanya ngoma kila siku japokuwa nina uwezo wa kuachia ngoma mfululizo.” – Ben Paul.
“Ili thamani yangu iendelee kuwa palepale na kuongezeka zaidi ni lazima nichukue muda mwingi sana kufikiri nini kinahitajika kwenye soko la mziki wetu na wenzangu hawafanyi, so hali hii ya uwepo wa artists wengi wenye uwezo na kiu ya mafanikio si ya kukurupuka na kutoa ngoma tu. Lazima ufikiri sana ndo ufike pale unapopataka.” – Ben Paul.
Pia alimaliza kwa kusema kuwa kwenye muziki kuna hitaji utulivu wakati unapotaka kutunga wimbo kwakuwa unaweza ukajikuta una rudia vitu ambavyo tayari umekwisha vitoa au wenzako wamefanya.

No comments: