DJ BOSTON-ON BEAT U KNOW WAT IT IS!!!

Sunday, January 5, 2014

Project Ya Tanzania Bila Dawa Kuanzishwa Na Kala Pina Mwezi March 2014

pina 
 Msanii mkongwe wa Hip Hop na kiongozi wa kundi la Hip Hop lijulikanalo kwa jina la Kikosi cha Mizinga… Kala Pina, ameandaa project nyingine ya Tanzania Bila Dawa itakayo anza rasmi mwezi wa tatu mwaka huu 2014 baada ya project ya Hip Hop Bila Madawa kuleta mafanikio. Msanii huyu amesema kuwa project hii ya sasa inalenga kuelezea kilio cha wasanii katika kupiga vita biashara haramu ya madawa yakulevya ambayo tayari imeshaenea katika maisha ya baadhi ya wasanii na inazidi kuangamiza maisha ya vijana ambao ndio nguvu kazi ya taifa katika maendelo ya nchi yetu.

http://www.gongamx.com/wp-content/uploads/2014/01/madawa-ya-kulevya.jpg 
 Hip Hop Bila Madawa Ilikuwa project ambayo inalenga wasanii na vijana walioko katika harakati za Hip Hop, na sasa Kala Pina ameamua kuleta project pana zaidi ambayo itajumuisha wasanii wote na Taifa letu kiujumla, na ndomana project hii mpya itaitwa Tanzania Bila Dawa. Project hii itakayo zinduliwa rasmi mwezi March mwaka huu wa 2014 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es saalam  na baadae kusambaa kwenye miji mengine kama Mwanza, Arusha na mikoa mingine pia ina lengo la kuchangisha fedha ili kuweza kuwasaidia vijana wengineo ambao tayari wamesha athirika na matumizi ya madawa ya kulevya hapa nchini.

No comments: