DJ BOSTON-ON BEAT U KNOW WAT IT IS!!!

Saturday, April 12, 2014

Chupa jipya la Dimpoz kukamilika mwezi huu

 

 Staa wa muziki wa Bongoflava, Ommy Dimpoz amewaahidi mashabiki wake kuachia kazi mpya ambayo itakuwa gumzo la Jiji hivi karibuni ikiambatana na video ambayo amewekeza pesa nyingi kuifanya huko nchini Uingereza, kazi ambayo itakuwa tayari mwezi huu.

 
Kuhusiana na kazi hii mpya ambayo picha zake zimekwisha onekana mitandaoni, Dimpoz ameweka wazi kuwa imekuwa ni somo kubwa kwake kufanya kazi hii iliyo katika kiwango cha kimataifa, akiwa chini ya uongozaji wa mtayarishaji video mkubwa kabisa, Moe Musa ambaye anafanya kazi zake huko Uingereza.
Ommy Dimpoz amesema kuwa, kutokana na kiasi cha pesa ambacho amewekeza katika video hii, muda na kufuatilia mpangilio wa ratiba ya kazi bila kuweka utani, kazi hii itaacha gumzo hapa Tanzania na Afrika kwa ujumla pindi itakapotoka.


No comments: