DJ BOSTON-ON BEAT U KNOW WAT IT IS!!!

Thursday, March 27, 2014

Kigwema ajipanga kurudi nyumbani

 

 Kigwema ambaye kwa sasa amekuwa kimya katika muziki amedai ameamua kuanza na project ya Narudi nyumbani ambayo itakuwa maalumu kwa watu wa kusini kabla ya kuachia kazi mpya aliyofanya na Stara Thomas.
"Nilipanga kuachia wimbo wangu mwezi wa tatu lakini kuna wadau wa muziki na wasanii wakongwe walinipa maoni yao na kunishauri hiyo kazi niifanye kwa P Funk nikasikiliza maoni yao na nimeanza kuyafanyia kazi lakini nimeona nisiwe kimya ndio maana nimekuja na Project ya Narudi nyumbani ambayo hii project imelenga watu wangu wa kusini kwa kuwa muda mwingi niko kule hivyo nisikae kimya muda wote mkapa hapo kazi yangu mpya itakapotoka"
Akizungumzia project narudi nyumbani amedai kuwa kuanzia Jumamosi wataanza kutengeneza Video ya narudi nyumbani na wataanzia Somanga mpaka Mtwara na hii yote ni kushow upendo wa watu wake wa kusini ambao muda mwingi wamekuwa wakimpa hamasa ya kufanya kazi nzuri zaidi na kumfanya afurahie kuishi kusini.
Kigwema alishawahi kutamba na nyimbo mbalimbali ikiwemo Sintomshau,Kwenye magazeti na zingine nyingi.

No comments: