DJ BOSTON-ON BEAT U KNOW WAT IT IS!!!

Wednesday, March 26, 2014

Madee atoa malalamiko yake kwa BASATA, baada ya wimbo wake kuzuiliwa kuingia tuzo za KTMA

 
 
 
BAADA ya Baraza la Sanaa Taifa (BASATA), kuondoa nyimbo ya msanii wa muziki wa kizazi kipya Madee, nyimbo inayojulikana kwa jina la Tema mate Tuwachape, mapya yaibuka ambapo msanii huyo adai kuwa Baraza hilo limechelewa kufanya maamuzi.
Msanii huyo amedai kuwa baraza hilo limechelewa kufanya maamuzi hayo ya kuuondoa wimbo huo katika kinyg’aganyiro hicho ikiwa nyimbo hiyo imeshapigwa kwa muda wa mwka mzima sasa.
Madee ametoa ushauri kwa baraza hilo kuwa ni vyema wakaweka chombo maalumu cha kuhakiki nyimbo zao kabla hazijapelekwa kwa mashabiki hali hiyo itasaidia kurekebisha makosa.
Aliongezea kuwa kuondoa wimbo huo katika kinyanga’nyiro hicho hawajatenda haki kwani nyimbo yake imeshikiria chati kwa muda mrefu kwenye redio mbalimbali, hivyo ni sawa na kuwadhurumu mashabiki wake.
Alienda mbali zaidi ambapo anadai kuwa kauli hiyo ya kuondolewa haijamshtua sana kwani hajawahi kupokea tuzo yoyote tangu ameanza kazi ya muzi.
Nyimbo ya Madee, ni miongoni mwa nyimbo zilizoenguliwa katika mchakato wa kinya’nganyiro cha tuzo hizo.

No comments: