DJ BOSTON-ON BEAT U KNOW WAT IT IS!!!

Friday, September 13, 2013

 
 
Kundi maarufu la muziki nchini Kenya Sauti Sol linatarajiwa kukonga nyoyo za mashabiki katika tamasha kubwa lililobatizwa jina ‘Lake of Stars 
Festival’ litakalofanyika tarehe 27 na 28 mwezi huu nchini Malawi.
 
Bendi hiyo imealikwa katika project kubwa ambayo itakuwa inafanya sherehe za kumbukumbu ya miaka 10 ya uanzilishi wa kituo cha sanaa za muziki, filamu, maigizo, maonyesho mbalimbali yanayohusiana na kuutangaza utamaduni wa nchi hiyo duniani.
 
Aidha, tamasha hilo litasheheni wasanii na makundi mbalimbali barani Afrika wakiwemo Yadi, George the Poet, Sauti Sol, Tumi,Yolanda Kaluma, na wengineo wengi.

No comments: