DJ BOSTON-ON BEAT U KNOW WAT IT IS!!!

Wednesday, October 30, 2013

FIESTA NI ZAIDI YA FESTIVAL NDANI YA EAST AFRICA NZIMA. (PHOTOS)

 22


Tamasha kubwa la burudani linalofanyika kila mwaka likiwa na jina kubwa ‘FIESTA’ safari hii likiwa limepewa udhamini wa nguvu kutoka Serengeti Breweries Limited kupitia bia ya Serengeti, limevunja rekodi ya kuwa tamasha kubwa zaidi kuwahi kufanyika ndani ya Tanzania na ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Tamasha la Fiesta mwaka huu lilijumuisha mikoa 14 ambapo kwa mara ya kwanza ilihusisha mikoa ya Kigoma, Mwanza na Zanzibar huku semina za fursa zikizidi kuipa heshima tamasha hilo na kulifanya la tofauti zaidi lisilowahi kutokea duniani. Pia lilihusisha utolewaji wa zawadi kwa watu mbalimbali mikoani kama vile Pikipiki n.k.


chege 


dancers 



J-Martins 


Lina 


madee 


nay-wa-mitego

Kwa mara ya kwanza wasanii wa ndani zaidi ya hamsini na wa nje wanne (Davido,Iyanya, Alaine na Nonini) wamehusika kuupamba usiku wa tarehe 26/10/2013 na tarehe 27/10/2013 huku stage ya kimataifa iliyo katikati ya watu ikitoa fursa ya kila mtu kuona kinachoendelea jukwaani. Mbali na changamoto za hapa na pale zilizojitokeza hadi kupelekea tamasha hilo kufanyika kwa siku mbili, lakini lilifana sana na hata wale ambao hawakupata fursa ya siku ya kwanza kuhudhuria basi walitoa pongezi kwa maandalizi yaliyofanywa na kamati ya maandalizi ya Fiesta.
Shukrani na pongezi za kipekee ziende kwa uongozi mzima wa Clods Fm na kila aliyeshiriki kufanikisha tamasha hilo ikiwemo kampuni ya bia Tanzania Serengeti Breweries Ltd.

No comments: