DJ BOSTON-ON BEAT U KNOW WAT IT IS!!!

Tuesday, November 19, 2013

Dalilah amekuja kuwashika

 
Msaniii wa muziki wa kizazi kipya ambaye ameamua kuzama katika miondoko ya muziki aina ya zouk Dalilah Led, amefyatua kichupa chake kipya 'Sitaki Maneno' kilichotambulishwa kwa mara ya kwanza East Africa Television.

Mbali na kazi hii, Dalilah amesema kuwa anawafagilia sana madiva wanaofanya muziki wa aina hiyo huku akimwagia sifa kemkem mwanadada Lady Jaydee pamoja na K-Lynn akisema kuwa ni wasanii ambao amekuwa akiwafuatilia kwa karibu na kupenda aina ya muziki wanaoufanya.

Msanii huyu amesema kuwa kazi hii ni mwanzo tu wa mambo mazuri kutoka kwake ambapo amewaomba mashabiki kukaa tayari kwa mfululizo wa kazi nzuri kutoka kwake.

No comments: