
Rapa huyu ambaye ameonyesha uwezo wa ajabu wa kuweza kufanya muziki katika kiwango cha hali ya juu na pia kuweza kuendelea na masomo mpaka ngazi hii ya juu, amesema kuwa malengo pamoja na kuwa na mpango ni moja kati ya mambo ambayo yamechangia katika mafanikio ambayo ameyapata mpaka sasa.
Nikki amesema kuwa, kwa sasa baada ya kumaliza masomo, amefikiria kuanzisha shughuli kadhaa ambazo anaziona kuwa zinaweza kumsaidia kuendesha maisha, ambapo amesema kuwa kwa nafasi ndogo sana anafikiria kupata ajira ama kuajiriwa, na muziki utaendelea kuwa ni kama mke wake ambaye hawatatengana mpaka mwisho wa maisha yake.
No comments:
Post a Comment