Belle 9, moja kati ya wasanii wenye vipaji vikubwa kabisa vya kuimba
hapa nchini Tanzania, ametolea ufafanuzi suala la albam yake ya Vitamin
Music kutokuingia sokoni katika muda ambao alikuwa amewaahidi mashabiki
wake, ambapo amesema kuwa suala hili limesababishwa na yeye kuwa kimya
kwa muda.
Belle 9 ambaye sasa amejipanga kurudi kwa kasi katika chati za muziki kwa kuachia ngoma kadhaa, akiwa tayari ametanguliza ngoma ya 'Wanitamani' amesema kuwa, albam yake ipo na itatoka mara tu baada ya yeye kujirudisha katika chati.
Msanii huyu amekiri changamoto ya kuzidiwa na majukumu hasa kutokana na ukweli kuwa kwa sasa anafanya kazi yake akiwa hana msimamizi/meneja yoyote, huvyo kumfanya kuwa mtendaji mkuu katika shughuli zote zinazohusu muziki wake.
Belle 9 ambaye sasa amejipanga kurudi kwa kasi katika chati za muziki kwa kuachia ngoma kadhaa, akiwa tayari ametanguliza ngoma ya 'Wanitamani' amesema kuwa, albam yake ipo na itatoka mara tu baada ya yeye kujirudisha katika chati.
Msanii huyu amekiri changamoto ya kuzidiwa na majukumu hasa kutokana na ukweli kuwa kwa sasa anafanya kazi yake akiwa hana msimamizi/meneja yoyote, huvyo kumfanya kuwa mtendaji mkuu katika shughuli zote zinazohusu muziki wake.
No comments:
Post a Comment