
Rapa Octopizzo wa nchini Kenya, ameripotiwa kutoa ya moyoni kuhusiana na
wasanii wenzake ambao wanafanya muziki wa Injili hususan huko nchini
Kenya, ambapo kwa mujibu wa mtazamo wake asilimia 70 ya wasanii hawa
hufanya muziki huu kwa malengo ya kupata pesa zaidi.
Octopizzo amesema hadharani kuwa wasanii hawa wamegeuza lengo la muziki wa injili kutoka katika kusambaza ujumbe mzuri wa Mungu kwenda katika biashara, na hivyo kuondoa tofauti ya muziki wa injili na muziki wa ki-dunia.
Muziki wa injili nchini Kenya umekuwa na kujijengea nafasi kubwa katika soko la muziki nchini Kenya na Afrika Mashariki huku kukiwa na tofauti ndogo katika mtindo wa mavazi na dansi, kitu ambacho kimepelekea wengi kuwa na mtazamo wa tofauti juu ya muelekeo wa muziki huo.
Octopizzo amesema hadharani kuwa wasanii hawa wamegeuza lengo la muziki wa injili kutoka katika kusambaza ujumbe mzuri wa Mungu kwenda katika biashara, na hivyo kuondoa tofauti ya muziki wa injili na muziki wa ki-dunia.
Muziki wa injili nchini Kenya umekuwa na kujijengea nafasi kubwa katika soko la muziki nchini Kenya na Afrika Mashariki huku kukiwa na tofauti ndogo katika mtindo wa mavazi na dansi, kitu ambacho kimepelekea wengi kuwa na mtazamo wa tofauti juu ya muelekeo wa muziki huo.
No comments:
Post a Comment