Baada ya majina ya waliochaguliwa kuingia katika nominations za tuzo
za Kili Tanzania Music Awards 2014 kutolewa wiki hii, wasanii na wadau
mbalimbali wamepokea kila mmoja kwa hisia tofauti. Mwimbaji wa ‘Sugua
Gaga’ Shaa ambaye hakufanikiwa kuingia amezungumzia jinsi alivyopokea
nominations hizo.
“Kwa jinsi ninavyosikia ni kwamba kura za wananchi hazikuzingatiwa,” Alisema Shaa kupitia Clouds E ya Clouds TV. “kwa asilimia kubwa kura za wananchi wale watu waliowapendekeza hazijazingatiwa, sijui kwanini na ningependa kujua kwanini kwasababu nilivyosikia vitetesi vya hapa na pale wimbo wa Sugua Gaga ulikuwepo, aah kwahiyo nataka kufahamu kwanini wananchi mmewahusisha wasuggest kwamba Shaa awepo na wimbo huu uwepo halafu kwanini basi mwisho wa siku hamjazingatia hilo.”
“Kwa jinsi ninavyosikia ni kwamba kura za wananchi hazikuzingatiwa,” Alisema Shaa kupitia Clouds E ya Clouds TV. “kwa asilimia kubwa kura za wananchi wale watu waliowapendekeza hazijazingatiwa, sijui kwanini na ningependa kujua kwanini kwasababu nilivyosikia vitetesi vya hapa na pale wimbo wa Sugua Gaga ulikuwepo, aah kwahiyo nataka kufahamu kwanini wananchi mmewahusisha wasuggest kwamba Shaa awepo na wimbo huu uwepo halafu kwanini basi mwisho wa siku hamjazingatia hilo.”
Shaa ameongeza kuwa hakuna kitu alichopoteza wala kuongeza kwa
kutopendekezwa na haijamuuma kutokuwa nominated katika Tuzo lakini
kinachomuuma ni kuwahusisha wananchi waliompigia kura na bado
asichaguliwe.
“Kuhusu msimamo wangu mimi mwenyewe kutokuwa nominated…mwisho wa siku
mi naangaliaga nina gain kitu gani kwenye nominations aah nipo kwenye
game huu ni mwaka wangu wa tano nimewahi kuwa nominated kwenye Kili
Awards mara tatu…kwangu mimi nikiangalia sijapoteza kitu chochote na
wala sija gain kitu chochote. Kwahiyo kwangu mimi kusema ukweli
haijaniuma…ukweli kabisa haijaniuma kilichoniuma ni hiyo tu kwamba
kwanini mwananchi, tena hata mimi nikachukua muda walivyokuwa wanasema
aah mbona nyie watu wenyewe hamuhamasishi watu, nikachukua muda wa
kumlipa mtu atengeneze flier ili nihamasishe mtu apige kura na huyo mtu
akaiona hiyo flier akatumia vocha. Kwahiyo kwangu mimi ni hicho tu
kilichoniuma kwamba kama system ilikuwa haihitajiki kwanini ilikuwepo
pale.” Alimaliza Shaa
No comments:
Post a Comment