
Chillah amewataka watu na wadau mbalimbali kutambua kuwa kufanya
kwake filamu sio kwa lengo la kuuza sura au kukimbia majukumu yake ya
muziki.
Chillah amesema kuna watu wanaodhani uamuzi wake wa kufanya filamu umetokana na kushindwa kufanya muziki.
Chillah amesema kuna watu wanaodhani uamuzi wake wa kufanya filamu umetokana na kushindwa kufanya muziki.
“Hakuna kinachoshindikana katika maisha,” ameiambia Bongo5. “Kama
kuna watu muhimu wananiambia nifanye filamu nitaendelea kufanya. JB na
Adam Kuambiana Director waliniambia kuna filamu ya kufanya ‘Hukumu Ya
Ndoa Yangu’ na bado JB aliambia niwe kwenye kampuni yake Jerusalem ili
tufanye mambo makubwa zaidi ila nikamwambia bado kwanza kwa sasa.
Japokuwa mimi si mtu wa filamu watu wengi wanapenda nifanye filamu.
Kwahiyo nashangaa baadhi ya watu wanadhani nimeenda kwenye filamu
kwaajili ya kuuza sura na kukimbia majukumu yangu ya muziki. Jamani mimi
ni msanii Mkubwa sana na nina uwezo mzuri wa kuimba na kufanya vitu
vizuri sana katika muziki. Kwahiyo nitaendelea kufanya muziki wangu
mzuri na kama nitahitajika kufanya filamu nitafanya.Lakini maisha yangu
nyuma ya pazia naweza sana kufanya filamu vizuri sana,na pia si
biashara.”
No comments:
Post a Comment