DJ BOSTON-ON BEAT U KNOW WAT IT IS!!!

Sunday, March 30, 2014

Wahu; Watoto kwanza muziki baadae

 
Msanii wa muziki wa nchini Kenya, Wahu ambaye sasa ni mama wa watoto wawili, amesema kuwa kwa sasa katika maisha yake, familia yake hususan malezi ya watoto wake ndio kitu cha kwanza kabisa anachopenda na kujali huku muziki ukifuatia.
 
 
Wahu amesisitiza kuwa, ameweka familia yake mbele kwasababu kwake linapokuja swala la malezi ya watoto, haijalishi muziki unalipa kiasi gani, haipo sahihi kulipa mtu mwingine kufanya kazi hii ka niaba yake.
Hata hivyo, kauli hii ya Wahu haimaanishi kuwa ameweka kando muziki, na maelezo haya ameyatoa baada ya kushuka jukwaani kutumbuiza katika onyesho huko Ngara, akionyesha kuwa ana mpango maalum wa kuhakikisha kuwa anasongesha vitu hivi viwili katika mpangilio.


 

UKIIKOSA SUNDAY FLEVA LEO...WATAKUCHEKAAAAA......!!!

Uskose kutegea sikio kipindi chako cha SUNDAY FLEVA toka GENN RADIO leo saa nane mchana kwa saa za marekani ya kati ,saa mbili usiku kwa saa za uingereza na saa nne usiku kwa saa za afrika mashariki kusikiliza kutoka kwenye simu yako bonyeza hapa:http://liveradio.gennmedia.com/live.mp3 na kuangalia live bonyeza hapa: http://gennmedia.com/index.php/live-stream-top
http://liveradio.gennmedia.com


..........................

Friday, March 28, 2014

Konshens kurejea tena Nai

 

Mkali wa miondoko ya Dancehall kutoka nchini Jamaica, Konshens kwa mara ya pili katika historia anatarajia kutua Jijini Nairobi kutumbuiza katika onyesho kubwa litakalofanyika tarehe 12 mwezi Aprili.

 
Ujio wa msanii huyu ni moja ya matukio makubwa kabisa katika historia ya burudani nchini Kenya, akiwa bado anafanya vizuri kabisa na ngoma kali kama vile Bounce, Walk n Wine, Gal a Bubble na nyinginezo.
Kwa upande mwingine, staa mwingine mkali wa Kimataifa wa miondoko ya Reggae, Gramps Morgan naye ametangaza kuwa, yupo tayari kabisa kwa ajili ya kufanya ziara kubwa Afrika, ambapo miongoni mwa nchi anazotazamia kuzifikia kwa burudani, Kenya vilevile Tanzania zinatokea kwenye orodha.

Thursday, March 27, 2014

OSTAZ JUMA AKAZIA UCHUMBA KWA JOHARI, ASEMA LAZIMA

 OSTAZ JUMA AKAZIA UCHUMBA KWA JOHARI, ASEMA LAZIMA

PENZI limekolea na kinachoonekana sasa kwa Ostaz Juma Namusoma ni kukazia penzi lake kwa mwanadada Blandina Chagula ‘Johari’ anayesumbua kwenye Bongo Muvi.

Habari zilizolifikia Amani kutoka kwa chanzo chetu zinasema kwamba Ostaz alifunga safari kwenda nchini Afrika Kusini kwa mapumziko mafupi lakini pia kumnunulia mpenzi wake huyo zawadi mbalimbali kwa lengo la kupalilia uchumba wao.
“Jamaa alikuwa Sauzi (Afika Kusini), aliondoka hapa tarehe 17 (Machi) na amerudi tarehe 21. Kamletea zawadi kibao lakini kubwa zaidi ni kamera kubwa, nzuri ya kisasa kwa ajili ya kerekodia filamu,” kilipasha chanzo hicho.
Amani lilifanikiwa kumpata Ostaz kwa njia ya simu, akafafanua: “Ni kweli nilikuwa Afrika Kusini. Kuhusu Johari, ni kweli si mke wangu? Nimemletea zawadi nyingi sana, achana na hiyo kamera unayosema.
“Lengo ni kuweka uchumba wangu na yeye sawa. Nilitamani sana kusafiri naye lakini sikutaka kufanya hivyo ili kuweka usawa, mke wangu asione nimeegemea zaidi kwa mke mdogo.”
Alipoulizwa kwa nini amemuita Johari mkewe, haraka alisema: “Ndoa ipo karibu, nimeshaamua Johari awe mke wangu wa pili. Wadau wasubiri waone, uzuri ni kwamba dini yangu si kikwazo.”
hagula ‘Johari’ anayesumbua kwenye Bongo Muvi.
Habari zilizolifikia Amani kutoka kwa chanzo chetu zinasema kwamba Ostaz alifunga safari kwenda nchini Afrika Kusini kwa mapumziko mafupi lakini pia kumnunulia mpenzi wake huyo zawadi mbalimbali kwa lengo la kupalilia uchumba wao.
“Jamaa alikuwa Sauzi (Afika Kusini), aliondoka hapa tarehe 17 (Machi) na amerudi tarehe 21. Kamletea zawadi kibao lakini kubwa zaidi ni kamera kubwa, nzuri ya kisasa kwa ajili ya kerekodia filamu,” kilipasha chanzo hicho.
Amani lilifanikiwa kumpata Ostaz kwa njia ya simu, akafafanua: “Ni kweli nilikuwa Afrika Kusini. Kuhusu Johari, ni kweli si mke wangu? Nimemletea zawadi nyingi sana, achana na hiyo kamera unayosema.
“Lengo ni kuweka uchumba wangu na yeye sawa. Nilitamani sana kusafiri naye lakini sikutaka kufanya hivyo ili kuweka usawa, mke wangu asione nimeegemea zaidi kwa mke mdogo.”
Alipoulizwa kwa nini amemuita Johari mkewe, haraka alisema: “Ndoa ipo karibu, nimeshaamua Johari awe mke wangu wa pili. Wadau wasubiri waone, uzuri ni kwamba dini yangu si kikwazo.”

HAWA NDIO WASANII WALIOTUMIA MADAWA WAKAACHA


Msanii wa Bongo Flava maarufu kama Q Chief ni mmoja ya wasanii waliowahi kuweka wazi na kukiri juu ya matumizi yake ya madawa ya kulevya,aliweza kujihusisha na matumizi ya madawa hayo hatari ya kulevya kwa kipindi cha miaka miwili mfululizo, jambo ambalo lilipelekea kushuka kwake katika ramani ya muziki.

Aliwahi kutesa na ngoma zake nyingi ikiwemo hit single yake iitwayo Zamani,Akiwa ni mmoja wa waasisi wa bongo fleva hapa Tzee, kwa kuweka mchango mkubwa wakufanya muziki wa bongo fleva upewe heshima yake.Baada ya kuingia katika janga hili la taifa kama ilivyo kwa wasanii walio wengi kwa sasa, iliweza kumrudisha nyuma kimaendeleo kwa miaka hiyo miwili . Baada ya muda kupita alijitangaza kufanikiwa kuacha matumizi hayo ya madawa makali yakulevya, na kusema kuwa kutumia muda mwingi katika ibada. “Sala, kusoma vitabu na kujiweka mbali na makundi mabaya ndio kumenisaidia kuacha kutumia madawa”, alisema qchief alipokuwa anaelezea kile kilichokuwa kinamsaidia hadi kufanikiwa kuachana na mswala hayo ya madawa yakulevya.Hadi hivi sasa qchilla yupo fiti na kurudi katika muziki wa bongo fleva.



 

 Aisha Madinda
Aisha Mbegu ‘Madinda’ ni msanii mwingine wa muziki wa dansi aliyewahi kukiri kusumbuliwa na matatizo ya matumizi ya dawa ya kulevya,yeye akiwa amesumbuliwa na tatizo hilo kwa muda mrefu kidogo,aliweza kukiri kuwa matumizi ya madawa yalimpelekea kupoteza ramani ya maisha kabisa,nakujikuta kurudi nyuma kimuziki.
Aisha madinda baada ya kuona kuwa,hakuna kinachoenda sawa katika mipango yake kimaisha, aliamua kwenda kutafuta utatuzi huo,nakujisalimisha katika hospitali ya taifa ya muhimbili, ndipo alipoweza kupata matibabu yake ambayo hadi sasa kufanikiwa kuacha kabisa matumizo hayo.Kutokana na juhudi zake za kupambana na madawa hayo aliweza kupata kazi ya uhamasishaji ,katika shirika la Kudhibiti Madawa ya Kulevya na Ukimwi(PHRP),iliyopo huko Kinondoni,kazi kubwa aliyokuwa nayo ni kutoa somo juu ya matumizi ya dawa za kulevya na athari zake na jinsi yakuziacha kwa waathirika waishio katika kituo hicho.


 
 Ray C
“I broke up with my ex,nikasema kwanza nimtoe huyu aliyeniletea balaa hili.Haata mama yangu aliona mabadiliko.I loved him so much woth all my heart,but then I had to let him,ilibidi aende cause yeye ndiye aliyeniletea balaa lote”alikiri ray C akielezea kile kilichosababisha yeye kuingia katika janga hili la madawa ya kulevya .Ray c ni mwanamuziki mkubwa sana katika ramani ya Bongo fleva, aliyeweza kushika nyoyo za mashabiki wengi wa kila rika,mbali na ujuzi wake wa kukata(kucheza) ,pia ni sauti yake ile nzuri ya kumtoa nyoka pangoni ,kitu kinachopelekea kuwa na mashabiki wengi wa kila pembe za Africa ya mashariki.”
Baada ya kujihusisha na maswala ya madawa,Ray c anakiri kuwa,alianza kuona mambo yake hayaendi sawa ,na kila afanyalo hafanikiwi,wakati yeye mwenyewe ni mwanamke wa kazi,ikabidi atafakari na kuanza harakati ya jinsi ya kutatua tatizo lake kwa kuwa alishajitambua kuwa madawa ya kulevya ndio yanayomrudisha nyuma kimaendeleo.
Ilikuwa si kazi rahisi kwake Ray C kupigana na gonjwa hilo,jambo lilomfanya kuhaha kila kona kutafuta matibabu,yaliyompeleka hadi Nairobi na baadaye kurudi hapa nchini Tanzania na kufanikiwa kupata matibabu katika hospitali yataifa yaliyompa matunda makubwa na hatua kubwa katika kupigana na ugonjwa huo.Hadi hivi sasa Ray c ameacha kabisa matumizi hayo na kufanikiwa kuanzisha Foundation yake mwenyewe ,inayosaidia waathirika wa madawa ya kulevya.


Kigwema ajipanga kurudi nyumbani

 

 Kigwema ambaye kwa sasa amekuwa kimya katika muziki amedai ameamua kuanza na project ya Narudi nyumbani ambayo itakuwa maalumu kwa watu wa kusini kabla ya kuachia kazi mpya aliyofanya na Stara Thomas.
"Nilipanga kuachia wimbo wangu mwezi wa tatu lakini kuna wadau wa muziki na wasanii wakongwe walinipa maoni yao na kunishauri hiyo kazi niifanye kwa P Funk nikasikiliza maoni yao na nimeanza kuyafanyia kazi lakini nimeona nisiwe kimya ndio maana nimekuja na Project ya Narudi nyumbani ambayo hii project imelenga watu wangu wa kusini kwa kuwa muda mwingi niko kule hivyo nisikae kimya muda wote mkapa hapo kazi yangu mpya itakapotoka"
Akizungumzia project narudi nyumbani amedai kuwa kuanzia Jumamosi wataanza kutengeneza Video ya narudi nyumbani na wataanzia Somanga mpaka Mtwara na hii yote ni kushow upendo wa watu wake wa kusini ambao muda mwingi wamekuwa wakimpa hamasa ya kufanya kazi nzuri zaidi na kumfanya afurahie kuishi kusini.
Kigwema alishawahi kutamba na nyimbo mbalimbali ikiwemo Sintomshau,Kwenye magazeti na zingine nyingi.

(COMING SOON) PROF. JAY FEAT. DIAMOND PLATNUMZ – KIPI SIJASIKIA


































Joseph Haule aka Prof. Jay baada ya kuwa kimya sasa anakuja na ngoma yake ya ‘Kipi Sijasikia’ akimshirikisha mkali mwingine wa Bongo flava Diamond Platnumz.

Wimbo wa Prof. Jay umefanyika katika studio ya Bongo Records chini ya producer P.Funk Majani.
Just wait na ujio wa Prof. Jay

Ommy Dimpoz ndani Muscat, Oman.

ommy 

 Ommy Dimpoz maarufu kama “Dimpoz” Kesho tarehe 28 March, anatarajia kutoa burudani kwa mara ya kwanza wakazi wa Muscat, Oman. Pia Dimpoz ameambatana Manager wake Mubenga pamoja na dancer wake..


MADEMU KWETU NO “MKUBWA NA WANAE BAND”


































Vijana wanne wanaunda Mkubwa Na Wanae Band Aslay, Maromboso, Becka 1 na Bella kwa sasa wanatamba na kibao chao cha “Ya Moto” wamekuwa gumzo kwa mtaani.

Kwa sasa kila mtu anawatambua kutokana na kazi nzuri wanazozitoa day to day ila tatizo limekuja kuwa wakali hao wamekuwa mwiba mtaani kwa mademu kutokana na umaarufu wao, mwandishi wa BK alivyozipata habari hizo alifanya kuwadodosa wakali hao na kusema.
“Kwanza walimshutumu Aslay kwamba alipata demu tulipoenda kufanya show Mtwara sisi tunakanusha madai hayo na sio kweli kwani kule tulienda kikazi tu na sio kwa ajili ya mapenzi wengi wametushutumu kuhusu hilo, ila ikifika wakati wa hayo mambo si tutawaambia kwani lazima tufikie hatua hiyo.”
Hivi karibuni wanatarajia ku-release single yao mpya inayoelezea tuzo ya mapenzi amepewe nanii ianayokwenda kwa jina la “APEWE NANI”.


Bob Junior awashangaa BASATA kwa walichokifanya kwa Snura, Madee na Jux

5e5dd8e6a59f11e3a8080e78bfefbac0_8 


Wasanii mbalimbali wameendelea kuulalamikia uamuzi wa BASATA wa kuwafungia Snura, Jux na Madee kushiriki katika tuzo za KTMA kwa kile kinachosemsekana Video zao kukinzana na maadili ya KiTanzania. Leo kupitia ukurasa wake wa Instagram Bob Junior ameamua kufunguka kuhusiana na swala hilo.
Bob Junior aliandika “SIJAONA HAKI/SABABU YA HIZI NYIMBO KUONDOLEWA NA BASATA @juma_jux #uzuri wako @snuramushi #nimevurugwa @madeeali #temamate Wasanii ndo tunatunga nyimbo ziendanazo na globallaization kwan vijana wanapenda kutuona tofauti kama niivyo wawe wana tutungia wenyewe nyimbo kwasababu wanao chambua nyimbo ni wazee wanachotaka nass tuwe wazee” 
Siku ya juzi ikiwa ni masaa machache tu baada ya uamuzi huo kutangazwa na BASATA Diamond alifunguka na kusema  Ikiwa kweli tunalengo la kutoipotosha kimaadili jamii yetu na vizazi vyetu pendwa, nafikiri ni vyema tungeanza kuzuia Video na nyimbo za kutoka nje, kuliko kuzuia nyimbo na video za nyumbani ambazo uchafu wake Haufikii hata robo ya uliopo kwenye Nyimbo zinazopewa kipaumbele toka nje… Hii ni sawa na kuzidi kuukuza mziki wa nje huku tukiudidimiza na kuua mziki wetu… Will the target of reaching our goals ever be achieved?? #Ni_Mtazamo_tu.”

 69d5fdaab5aa11e38753125b8789c25f_8

ALIKIBA ADAI HAUFAHAMU WIMBO UITWAO ‘ROSA’


 

Bila shaka kama wewe ni shabiki wa Alikiba hukujiuliza mara mbili kuupakua wimbo wa ‘Rosa’ ambao umesambaa wiki hii katika mitandao kama comeback ya star huyo aliyekaa kimya kwa muda mrefu.

Lakini cha kushangaza ni kuwa Alikiba mwenyewe hautambui wimbo huo sababu hauko kwenye orodha ya nyimbo alizowahi kurekodi na wala hafahamu mtu aliyeuimba.
Alikiba amesema amepigiwa simu na vituo vya redio vikimuuliza kuhusu wimbo wake mpya walioupata uitwao ‘Rosa’ lakini hana taarifa nao.
“Nyimbo zipo lakini sija release nyimbo…sijatoa nyimbo so far na sijui nani ameimba na sijawahi hata kuisikia” Alisema Alikiba alipozungumza na mtangazaji Renatus Kiluvya kupitia New Chapter ya Radio Free Africa.
“Sijawahi kuisikia na sitaki kutoa comment yoyote kwasababu navyojijua mimi first of all najikubali sana, la pili watu wananiambia niko unique afu surprise watu wananiambia nimetoa nyimbo sijui tumesikia nyimbo inaitwa Rosa yaani hiyo sijaelewa bado.” Alisema hit maker wa Cinderella.
Aliongeza kuwa kuna uwezekano kuwa kuna watu wamefanya makusudi kufake wimbo huo uonekane ni wake kutokana na ukimya wake, au wamefanya sayansi sauti isikike kama yake, au huyo aliyeimba ni role model wake ndio sababu kaamua kufanya hivyo.
“Wameona nimekaa kimya sana wakaona ngoja watoe nyimbo na wakatumia jina la Alikiba, it doesn’t make sense kama unatoa nyimbo unategemea kutoka kwa jina la mtu flani, I think ni trick moja ambayo imefanywa sielewi na nani lakini I don’t know if in a good way or bad way.”
Pia Ali K alizungumzia ujio wake mpya,
“Ujio wangu uko very soon, sasa hivi wakae tayari fans wangu na kilichonifanya nikae kimya kingi watajua ni kitu gani na watani understand kabisa maana ya kukaa kimya.”

Christian Bella kutambulisha bongo fleva

 

 wanamuziki kutoka “Malaika music band” Christian Bella ameamua kujitupa kufanya muzuki ambao utakuwa tofauti kidogo na muziki ambao amekuwa akifanya kwa miaka kadhaa,akiwa na lengo la kuleta ladha tofauti katika muziki wake na kuongeza mashabiki


Christian Bella alisema kuwa kwa sasa anaanza kutambulisha wimbo wake mpya ambao amemshirikisha msanii Ommy Dimpoz,wimbo ambao umefanywa katika studio za Combination Sound chini ya produza Man Walter.
Ni kweli nimefanya aina tofauti ya muziki kwa sasa natambulisha Bongo fleva niliyofanya na rafiki yangu Ommy Dimpoz,wimbo unaitwa 'Nani kama mama' na nitautambulisha mwezi April mwanzoni,nitatoa Audio na Video kwa pamoja ili mashabiki waweze kupata burudani na kupata kumsikia na kumuona Bella akifanya Bongo Fleva"
Christian Bella aliongeza kuwa huo ni mpango wake kwa sasa kuchanganya ladha katika muziki wake hivyo mashabiki wakae teyari tu kwani kuna wimbo wa RNB utafuata baada ya Nani kama mama,wimbo ambao anafikiri kufanya na mwanamuziki wa Rnb wa hapa nyumbani huku akichanganya na msanii mwingine wa Hip Hop.
Christian Bella alishawahi kuwa Prezidaa wa Bendi ya Akudo Impact 'Vijana wa Masauti' kwa miaka kadhaa kabla ya kuachana na Bendi hiyo na kuanzisha Bendi nyingine inayofahamika kama 'Malaika music band”.

(OFFICIAL VIDEO) MIKE TEE – I WANNA KNOW

[New Audio] Mabeste – Headache

beste 

 Brand new song kutoka kwa Rapper Mabeste -Headache, nyimbo imefanyika Uprise Music Studio, Produced by Mabeste, Mixing and mastering-Dupy.


Diamond katika mchakato kuwania Tuzo Za Kora

 

 Msanii Diamond Platnumz, ameendelea kuchana mawimbi katika anga la Afrika ambapo amefanikiwa kuingia katika orodha ya wasanii 20 Bora ambao wanafanya vizuri Afrika, watakaoingia katika kinyanganyiro cha kuwania tuzo za Kora.

 
Diamond katika orodha hii, anatokea sambamba na majina ya wasanii wakubwa Afrika, kama vile Oliver Mtukudzi, Fally Ipupa, Mafikizolo pamoja na wakali wengine wa muziki barani Afrika.
Kutokea kwa Diamond katika orodha hii, ni nafasi nyingine kubwa ya kuipeperusha bendera ya Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla, katika jukwaa la kimataifa.
Kwa sasa mchakato unaendelea kupitia ukurasa wa facebook wa Tuzo hizi, ambapo maoni mbalimbali ya mashabiki yanakushanywa kuhusiana na wasanii gani wanaokubalika zaidi, tayari kwa kuwapambaniza katika tuzo hizo kubwa.

SHAA AHOJI KWANINI HAJAWA NOMINATED KATIKA KTMA 2014


 SHAA AHOJI KWANINI HAJAWA NOMINATED KATIKA KTMA 2014

Baada ya majina ya waliochaguliwa kuingia katika nominations za tuzo za Kili Tanzania Music Awards 2014 kutolewa wiki hii, wasanii na wadau mbalimbali wamepokea kila mmoja kwa hisia tofauti. Mwimbaji wa ‘Sugua Gaga’ Shaa ambaye hakufanikiwa kuingia amezungumzia jinsi alivyopokea nominations hizo.

“Kwa jinsi ninavyosikia ni kwamba kura za wananchi hazikuzingatiwa,” Alisema Shaa kupitia Clouds E ya Clouds TV. “kwa asilimia kubwa kura za wananchi wale watu waliowapendekeza hazijazingatiwa, sijui kwanini na ningependa kujua kwanini kwasababu nilivyosikia vitetesi vya hapa na pale wimbo wa Sugua Gaga ulikuwepo, aah kwahiyo nataka kufahamu kwanini wananchi mmewahusisha wasuggest kwamba Shaa awepo na wimbo huu uwepo halafu kwanini basi mwisho wa siku hamjazingatia hilo.”
Shaa ameongeza kuwa hakuna kitu alichopoteza wala kuongeza kwa kutopendekezwa na haijamuuma kutokuwa nominated katika Tuzo lakini kinachomuuma ni kuwahusisha wananchi waliompigia kura na bado asichaguliwe.
“Kuhusu msimamo wangu mimi mwenyewe kutokuwa nominated…mwisho wa siku mi naangaliaga nina gain kitu gani kwenye nominations aah nipo kwenye game huu ni mwaka wangu wa tano nimewahi kuwa nominated kwenye Kili Awards mara tatu…kwangu mimi nikiangalia sijapoteza kitu chochote na wala sija gain kitu chochote. Kwahiyo kwangu mimi kusema ukweli haijaniuma…ukweli kabisa haijaniuma kilichoniuma ni hiyo tu kwamba kwanini mwananchi, tena hata mimi nikachukua muda walivyokuwa wanasema aah mbona nyie watu wenyewe hamuhamasishi watu, nikachukua muda wa kumlipa mtu atengeneze flier ili nihamasishe mtu apige kura na huyo mtu akaiona hiyo flier akatumia vocha. Kwahiyo kwangu mimi ni hicho tu kilichoniuma kwamba kama system ilikuwa haihitajiki kwanini ilikuwepo pale.” Alimaliza Shaa

Bongo Fleva watakata viuno-H Baba

 

 Msanii wa muziki wa kizazi kipya Hamisi Ramadhani Baba,maarufu kama 'H.Baba' amefunguka na kusema kuwa wanamuziki wa Bongo fleva sasa watakata mauno,H Baba alisema hayo alipokuwa akihojiwa na EATV.


H Baba amesema kuwa wakati anatambulisha muziki wa Bongo Bolingo Fleva wadau wa mauziki kama hawakuweza kumuelewa na hawakuweza kumpa support ili muziki huo ufike sehemu nzuri zaidi lakini anashukuru sasa aina ya muziki aliokuwa akiupigania miaka kadhaa nyuma ndio umeliteka soko la muziki wa Afrika na unazidi kukua kwa kasi kubwa.
"Wakati nimeanza kufanya Bongo Bolingo Fleva watu hawakunielewa nafanya nini na kuna baadhi ya wasanii wenzangu walikuwa wakinikashifu kuwa H Baba yule ni mkata viuno tu,sasa kwa kuwa muziki huu ndio umeshika chat kwa sasa amini usiamini wasaniii wa Bongo Fleva sasa watakata viuno kama H Baba maana muziki huu unahitaji uwezo wa hali ya juu katika steji ndio maana hata watu ambao wanaufanya wapo vizuri stejini".
H Baba aliongeza kuwa kwa sasa wasanii wakubwa Africa kama P square,Iyanya,Davido na wengine wengi wanafanya muzuki ambao yeye anafanya hivyo kwa kuwa wasanii wengi wamekuwa si wabunifu kubuni vitu vyao hivyo wataanza kufanya huo muziki ila wanapaswa tu kuelewa kuwa muziki huo unahitaji uwezo mkubwa stejini.
Mimi nashukuru sana P Square kuweza kutoa wimbo wao huu wa Test my money ambao umekuwa na vionjo vya bolingo kama ambavyo mimi nafanya Bongo Bolingo fleva maana wimbo huu utasidia aina ya muziki huu kukua na kuenea zaidi na hii itanisaidia mimi maana wao watakuwa wamefanya kazi rahisi kuwaelewesha wadau juu ya aina hii ya muziki ninao fanya hivyo inaweza kunipa nafasi kufanya mambo mazuri zaidi,hivyo hawa wasanii wa Bongo fleva najua watafanya huu muziki lakini wanapaswa kutambua kuwa uhahitaji uwezo wa hali ya juu ukiwa stejini,hivyo wajipange kukata mauno tu.
Akizungumzia Wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Tubebane,H Baba amedai kuwa wimbo huo hakuutambulisha bali umevuja baada ya gari yake ndogo kuvunjwa kioo na kuibwa kwa baadhi ya vitu ikiwemo Flash ambayo ilikuwa na wimbo huo ndipo ilivuja,amedia kuwa haukuwa wakati wake kuachia wimbo huo kwa sasa kwa kuwa bado alikuwa akiendelea kujiandaa ili kuja kutambulisha wimbo huo siku za usoni.

[ New Video ] Mike ft Joh Makini – Likizo

WANAFANANA ILA SI AGNESS MASOGANGE

WANAFANANA ILA SI AGNESS MASOGANGE 

 Kupitia mitandao mingi wameweka picha inayomuonesha Agnes Masogange akiwaachia mgongo ila ukweli si Agness bali ni picha ya msichana mwingine mwenye mgongo kama video queen huyo.

Video queen huyo wa Msambinungwa, amepost picha hiyo inayomuonesha mdada mwenye mgongo anayefanana naye pia ni mrefu kuliko Agness.


Wednesday, March 26, 2014

JOSE CHAMELEONE KUTANGAZA UTALII WA UGANDA

JOSE CHAMELEONE KUTANGAZA UTALII WA UGANDA 

 Jose Chameleone amekabidhiwa rasmi jukumu la kutangaza utalii wa nchini Uganda, hususan vivutio zaidi ya 40 ambavyo vipo huko Busoga nchini humo.
Muimbaji huyo wa ‘Tubonge’ amepewa jukumu hilo na Spika wa Bunge la nchini Uganda, Rebecca Kadaga.

Kupitia Facebook, Chameleone ameandika: It’s evidential that music is a global language and is also a tool that is relevant to today’s society unlike the past where Musicians were not respected in sects of development. Today’s morning was a a fruitful one as I was at the Parliament of Uganda in a board meeting with Hon. Speaker of Parliament of Uganda, Hon.REBECCA KADAGA, Hon. Edward Baliddawa and the various honourables as they nominated me to be the esteemed AMBASSADOR of BUSOGA TOURISM”


 

 Pia mbali na ubalozi amekabidhiwa ubalozi wa shindano maalum la kutangaza utalii la Kupanda Mwamba wa Kagulu katika Mkoa wa Buyende kwa mwaka huu, ambapo watu mbalimbali watashiriki shindano hilo tarehe 9 na 10 May, 2014.


VIDEO YA HARUSI YA PAUL OKOYE WA P SQUARE

 VIDEO YA HARUSI YA PAUL OKOYE WA P SQUARE

Jumamosi iliyopita (March 22) pacha wa kundi la muziki P-Square, Paul Okoye na mpenzi wake wa muda mrefu Anita walifanya harusi ya kimila huko Port Harcourt iliyohudhuriwa na mastar wengi wa Nigeria.

Tazama kipande kidogo cha video ya harusi hiyo ambayo pia ilirushwa live na kituo cha Hip Tv cha Naija.


[ New Video ] Joe Candy – Nice and Slow

Amani hajaamua aende wapi?

 

 Msanii mkongwe wa muziki kutoka nchini Kenya, Amani amekataa kuweka wazi mipango ya muziki wake pamoja na usimamizi wake.


Hii ni baada ya lebo ya Ogopa ambayo amefanya nayo kazi kutoka mwaka 1999 alipoanza biashara ya muziki, kusitisha mikataba na wasanii wake wote mwanzoni mwa mwaka.
Amani amesema kuwa, hawezi kujadiliana kuhusiana na suala hili katika wakati huu bila kuweka
wazi sababu ya kufanya hivyo, ingawa imefahamika kuwa kwa sasa yupo katika mpango wa kurejea kwa mara nyingine katika muziki kwa kishindo.
Amani wiki kadhaa zilizopita, pia alinukuliwa akisema kuwa, ni kitu kizuri kukaa nje ya muziki
kwa muda ili kuweza kuweka mpango mzuri wa kurudi vizuri.


SKIDE NA DIAMOND PLATNUMZ ZIMEANZA KUIVA


 SKIDE NA DIAMOND PLATNUMZ  ZIMEANZA KUIVA

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Shamte Skide Nasibu,ambyea ana umri wa miaka 18 aliye ingia kwenye game la muziki Rasimi 2007 kwa kuanza na ngomayake ya ‘Vikindu’na kutamba kwa ngoma ya ‘Diamond kabla hajatoka’

Ikiwa kwa sasa ana jumla ya nyimbo7 na ngoma ilio mtoa ni ‘Diamond kabla hajatoka’,amedai kuwa Diamond ni ndugu yake wa damu,kwa upande wa baba.
“Diamond ni bother wangu kabisa siokwamba najipendekeza tume changia Baba Mama tofauti kutokana na mzee wetu Nasibu hakuwa mtu wakutulia, hikindicho kilicho tokea baina yangu na Diamond platnumz lakini kwasasa nashukuru kidogo uhusinowetu ukopoa tofautina zamani ilikuwa hata ni kimpigia sim hapokei lakini sasahivi tunawasiliana kamakawaida ingawa hakuna sapoti yeyote alionipa tofauti na kuwa Real model wangu kwenye game.


Madee atoa malalamiko yake kwa BASATA, baada ya wimbo wake kuzuiliwa kuingia tuzo za KTMA

 
 
 
BAADA ya Baraza la Sanaa Taifa (BASATA), kuondoa nyimbo ya msanii wa muziki wa kizazi kipya Madee, nyimbo inayojulikana kwa jina la Tema mate Tuwachape, mapya yaibuka ambapo msanii huyo adai kuwa Baraza hilo limechelewa kufanya maamuzi.
Msanii huyo amedai kuwa baraza hilo limechelewa kufanya maamuzi hayo ya kuuondoa wimbo huo katika kinyg’aganyiro hicho ikiwa nyimbo hiyo imeshapigwa kwa muda wa mwka mzima sasa.
Madee ametoa ushauri kwa baraza hilo kuwa ni vyema wakaweka chombo maalumu cha kuhakiki nyimbo zao kabla hazijapelekwa kwa mashabiki hali hiyo itasaidia kurekebisha makosa.
Aliongezea kuwa kuondoa wimbo huo katika kinyanga’nyiro hicho hawajatenda haki kwani nyimbo yake imeshikiria chati kwa muda mrefu kwenye redio mbalimbali, hivyo ni sawa na kuwadhurumu mashabiki wake.
Alienda mbali zaidi ambapo anadai kuwa kauli hiyo ya kuondolewa haijamshtua sana kwani hajawahi kupokea tuzo yoyote tangu ameanza kazi ya muzi.
Nyimbo ya Madee, ni miongoni mwa nyimbo zilizoenguliwa katika mchakato wa kinya’nganyiro cha tuzo hizo.

AY AFANYA TANGAZO LA SAMSUNG

Mafikizolo kudondoka Dar April

 
 Kundi maarufu la Muziki kutoka Afrika Kusini, Mafikizolo linatarajiwa kudondosha burudani ya aina yake itakayoacha gumzo Jijini Dar es Salaam, katika ukumbi wa Mlimani City tarehe 5 mwezi Aprili mwaka huu.


Mafikizolo ambayo inaundwa na wakali Theo Kgosinkwe na Nhlanhla Nciza tayari wamejipanga vilivyo kwa ajili ya kulishambulia jukwaa katika onyesho ambalo linakuwa ni la kwanza kabisa kulifanya haba Bongo katika historia ya kundi hili.
Tiketi za onyesho hili linalosubiriwa kwa hamu, zinapatikana kwa shilingi 20,000 tu katika maeneo na mlangoni siku ya tukio, tiketi hizi zitapatikana kwa shilingi 35,000.



[ New Video ] Mike Tee – I wanna know

Mike-T 


Daddy Owen kuandaa mashindano

http://www.eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/field/image/daddy-owen1.jpg?itok=zTCW8taJ 

 Msanii Daddy Owen wa nchini Kenya, baada ya kushuhudia mafanikio makubwa kupitia muziki
anaofanya, ameamua kusherekea na mashabiki kwa namna yake kupitia mashindano makubwa ya mpira wa miguu ambayo atayaandaa hivi karibuni.


Daddy Owen ambaye pia yuko katika mpango wa kuoa mwishoni mwa mwaka huu, amesema kuwa, michuano hii ya mpira wa miguu atakayoianzisha hivi karibuni, itawapatia nafasi wapenzi wa mchezo huu kuhudhuria na kupata burudani ya kutazama kabumbu moja kwa moja na bure kabisa.
Daddy Owen amesema kuwa, uamuzi hii ni kufuatia suala lililo wazi kuwa, mchezo wa mpira wa miguu umekuwa na mashabiki wengi, ila asilimia kubwa wanashindwa kupata nafasi ya kuuona mchezo huu moja kwa moja kutokana na gharama za kiingilio ambazo hawazimudu.




PICHA ZA UTATA ZA MWANADADA HUDDAH KUTOKA KENYA

 

 Mwanadada Huddah kutoka Kenya akiwa katika pozi mbali mbali mbali za uchokozi.



 



Ile video iliyo wakutanisaha wasanii 19 kutoka Afrika wakiwemo AY na Diamond kutoka March 31

d65b88e4a6e311e38b4f1280e484f25a_8 


Ile video iliyokua ukisubiliwa kwa hamu, iliyojumuisha wasanii wakubwa 19 kutoka pande mbalimbali za Afika na kufanyika huko nchini Afrika Kusini itatoka rasmi Tarehe 31 ya mwezi huu. Wasanii kutoka Tanzania waliotuwakilisha katika video hiyo ni AY na Diamond Platnumz.
Mastar wengine ni Victoria Kimani,DBanji wa Nigeria,Vusi Nova South Africa,Femi Kuti Nigeria na Wengine wengi. Walioandaa ni Project hiyo ni shirika la One, huku lengo kubwa la kuwakusanya wasanii hao likuwa ni kuandaa wimbo mmoja ambao kupinga njaa katika bara la Afrika.


Kenzo kusimamiwa na kampuni kutoka Dubai

 

 Msanii Kenzo kutoka nchini Kenya, baada ya kutangaza kuwa mambo yake sasa yameanza kumnyookea baada ya kutoka chini ya usimamizi ya lebo ya Ogopa, ameweka wazi kuwa kwa sasa yupo katika hatua za mwisho za makubaliano kuingia katika mkataba huo.



Kenzo amesema kuwa, katika mkataba huu mpya atakaoingia, atakuwa na uhuru wa kurekodi kazi zake sehemu nyingine yoyote ile, tofauti na mkataba wa awali ambao ulikuwa ukimbana kufanya kazi sehemu moja.
Endapo mipango hii ya Kenzo itanyooka kama matarajio yake yalivyo, itakuwa ni nafasi nyingine kubwa ya msanii huyu kuweza kufanikiwa kuingia kwa nguvu katika soko la muziki la Kimataifa.


K MSANII KUTOKA ZAMBIA AME-LAUNCH PERFUME ZAKE BONGO

JK MSANII KUTOKA ZAMBIA AME-LAUNCH PERFUME ZAKE BONGO

Msanii anaye-hit’ na masong yake East and Central Afrika anayefahamika kama JK kwa sasa anabamba na wimbo wake wa ‘Telemonde lovin’ na zingine kibao.

JK ni msanii anayefahamika sana Afrika ya Kati kutokana na ngoma zake ku-bang sana pande hizo,kwa sasa yupo Bongo kibiashara pamoja na kazi ya kimuziki, hivi sasa JK ameweza ku-launch manukato yake aina ya ‘Hot Ice’.

Diamond awalalamikia Basata, baada ya kuziondoa nyimbo za Jux, Madee na Snura kwenye Tuzo za KTMA

a38085d0a87a11e398200e56170da01a_8 


Yakiwa yamepita masaa machache tu tangu Basata watangaze majina yatayowania Tuzo za KTMA 2014. Diamond ameamua kufunguka na kulaani kitendo kilichofanywa na Basata cha kuwafungia Jux, Madee na Snura kutokana tu na video zao kuonekana hazikizi maadali ya Kitanzania.
Kupitia akaunti yake ya InstagramDiamond aliandika “Ikiwa kweli tunalengo la kutoipotosha kimaadili jamii yetu na vizazi vyetu pendwa, nafikiri ni vyema tungeanza kuzuia Video na nyimbo za kutoka nje, kuliko kuzuia nyimbo na video za nyumbani ambazo uchafu wake Haufikii hata robo ya uliopo kwenye Nyimbo zinazopewa kipaumbele toka nje… Hii ni sawa na kuzidi kuukuza mziki wa nje huku tukiudidimiza na kuua mziki wetu… Will the target of reaching our goals ever be achieved?? #Ni_Mtazamo_tu.”
Fans wa Diamond Instagram nao hawakuakaa kimya na kuamua kumuunga mkono Diamond, na hizi ni baadhi ya maoni waliyotoa.
minaemmy Yaaan nachokiona mm naona wanataka kuua kizazi hiki cha mziki na cio fresh mm cio msaani ila imeniuma kweli!
marwamnanka Ukiona mtoto wako anaharibika na anaemuharibu ni wa jirani anza kwaza kumzuia wa jirani acje nyumbani then ndo umzuie na wa kwako
ashurayusuph Kweli kabisaaa wala hujakosea wenzetu hata uchi wanacheza muziki au filam tunaletewa na tunaangalia wala hazifungiwi kunya anye kuku akinya bata et kaarisha


Ditto awapa somo Wasanii

 

 Msanii wa muziki Lameck Ditto, ametoa ushauri wa bure kwa wasanii wenzake kujaribu kuangalia namna ambavyo wanaweza kutumia vipato wanavyotengeneza katika muziki, kuwekeza katika miradi na shughuli mbalimbali, na kuacha kuendekeza starehe.



Ditto amesema kuwa, kwa hulka yake binafsi anaona kuwa kuna umuhimu mkubwa wa kuwekeza na kuongeza njia za vipato, ambapo yeye binafsi amekwishaanza kuonyesha mfano kwa kujishughulisha na kilimo pamoja na shughuli nyingine ambazo zinamsaidia kuendesha maisha yake vizuri.
Huyu hapa Ditto mwenyewe akimwaga somo hili kali kwa wenzake;

SIFANYI FILAMU KUUZA SURA – Q CHILLAH



 

Chillah amewataka watu na wadau mbalimbali kutambua kuwa kufanya kwake filamu sio kwa lengo la kuuza sura au kukimbia majukumu yake ya muziki.

Chillah amesema kuna watu wanaodhani uamuzi wake wa kufanya filamu umetokana na kushindwa kufanya muziki.
“Hakuna kinachoshindikana katika maisha,” ameiambia Bongo5. “Kama kuna watu muhimu wananiambia nifanye filamu nitaendelea kufanya. JB na Adam Kuambiana Director waliniambia kuna filamu ya kufanya ‘Hukumu Ya Ndoa Yangu’ na bado JB aliambia niwe kwenye kampuni yake Jerusalem ili tufanye mambo makubwa zaidi ila nikamwambia bado kwanza kwa sasa. Japokuwa mimi si mtu wa filamu watu wengi wanapenda nifanye filamu. Kwahiyo nashangaa baadhi ya watu wanadhani nimeenda kwenye filamu kwaajili ya kuuza sura na kukimbia majukumu yangu ya muziki. Jamani mimi ni msanii Mkubwa sana na nina uwezo mzuri wa kuimba na kufanya vitu vizuri sana katika muziki. Kwahiyo nitaendelea kufanya muziki wangu mzuri na kama nitahitajika kufanya filamu nitafanya.Lakini maisha yangu nyuma ya pazia naweza sana kufanya filamu vizuri sana,na pia si biashara.”


YOUNG KILLER APOTEZA MARAFIKI

 

 anii Young Killer ambaye amerudi kwa kasi katika chati za muziki na ngoma yake mpya ambayo inakwenda kwa jina “My Power” ambayo amemshirikisha Damiani Soul, amesema tangu afahamike na wengi kupitia muziki, amepoteza idadi kubwa ya marafiki.

 Tofauti na wengi walivyotegemea, Young Killer amesema kuwa, Muziki umempunguzia marafiki, lakini pia rapa huyu akakiri kuwa muziki huu huu umemkutanisha na kumpatia nafasi ya kufahamiana na watu wengi.
Young Killer pia amezungumzia ukali wa ngoma zake ambapo amesema kuwa, yeye hutumia muda mrefu sana katika kuandika mashairi ya muziki wake, kitu ambacho kinafanya mashairi yake kukubalika kwa kiasi kikubwa kila kukicha na idadi kubwa ya watu.


Haya ndio majina ya wanaowania Tuzo za KTMA 2014


 BASATA

Baraza la sanaa la Taifa (BASATA)Leo limetangaza rasmi matokeo ya mchakato mzima wa kuwapata wateule rasmi wa vipengele 34 vya Tuzo za muziki Tanzania.Akiongea na waandishi wa habari Kaimu Katibu Mtendaji wa BASATA,Godfrey .L.Mngeleza alisema , zaidi ya mapendekezo 30,000 yalitumwa kwa njia ya sms na mtandaoni.Hata hivyo alidai kuwa nyimbo ‘Uzuri wako’ ya jux,’nimevurugwa’ ya Snura na ‘tema mate tuwachape’ ya Madee zimeondolewa katika mchakato huo kwa madai kuwa zimevunja maadili na hazifai kwa jamii ya Tanzania.

Screen-Shot-2014-03-25-at-11.59.09-AM 

 
Nyingine ni
WIMBO BORA WA AFRIKA MASHARIKI – Tubonge ya Jose Chameleone, Nakupenda pia ya Wyre na Alaine, Badilisha ya Jose Chameleone, Kipepeo ya Jaguar, Kiboko changu ya Amani, Weasal na Radio.
WIMBO BORA WA TAARAB – Wasiwasi wako wa Mzee Yusufu, asie kujua hakuthamini Isha na Saida Ramadhani, Nipe stara Rahima Machupa, sitaki shari Leila Rashid, fahari ya mwanamke ya Khadija Kopa, mambo bado Khadija Yusufu, kila muomba Mungu ya Mwanahawa Ally.
WIMBO BORA WA RAGGA/DANCEHALL – Nishai ya Chibwa ft Juru, Sexy Lady ya Dr. Jahson, My sweet ya Jettyman Dizano, feel alright ya Lucky Stone na wine ya Princess Delyla.
WIMBO BORA WA KUSHIRIKISHWA/KUSHIRIKIANA – Muziki gani ya Ney wa Mitego ft Diamond, Joto hasira ya Lady Jaydee ft Prof J, kidela ya Ally Kiba na Abdu Kiba, bila kukunja goti ya MwanaFA, Ay ft J Martins na tupogo ya Ommy Dimpoz ft J Martins.
RAPA BORA WA MWAKA WA BENDI – Kitokololo, Chokoraa, Ferguson, Canal Top na Totoo ze bingwa.
MTUMBUIZAJI BORA WA KIKE WA MUZIKI – Khadija kopa, Vanessa Mdee, Isha Ramadhani, Luiza Mbutu, Catherine (Cindy)
MTAYARISHAJI BORA WA NYIMBO WA MWAKA TAARAB – Enrico, Ababuu mwana wa Zanzibar na Bakunde.
MTAYARISHAJI BORA WA NYIMBO WA MWAKA (BENDI) – Allan Mapigo, C9, Enrico, Amoroso na Ababuu mwana wa Zanzibar.
WIMBO BORA WA REGGAE – Niwe nawe ya Dabo, hakuna matata ya Lonka, tell me ya Dj Aron ft Fidempha, bado nahitaji ya Chikaka ft Bless P & Lazzy B, Bongo reggae ya Warriors from the east.
WIMBO BORA WENYE VIONJO VYA ASILI YA KITANZANIA – Kwejaga nyangisha ya Batarokota, Nalonji ya Kumpeneka, bora mchawi Dar bongo massive, tumbo lamsokota ya Ashimba, Aliponji ya Wanakijiji na Agwemwana ya Cocodo african music band.



Credit : Millard Ayo

[ New song ] Rapdamu and Cannibal – Friday Fever

ni rapdamu 1 


Linex, Jambo Squad wafanya jambo

 

 sanii wa muziki, Linex Sunday Mjeda, baada ya kusumbua sana katika chati mbalimbali za muziki na ngoma yake ya Kimugina, kwa sasa ameamua kuunganisha nguvu na Jambo Squad kutoka Arusha kupitia kolabo ambayo imesukwa chini ya studio za Noize Makers.


Linex ambaye katika rekodi za muziki wake, hii inakuwa ni kazi ya kwanza kabisa kufanya na wasanii kutoka Arusha ikiwa pia ni aina tofauti kabisa ya muziki ambayo amewahi kufanya.
Kazi hii itatoka hivi karibuni ikiwa na matarajio makubwa ya kuunganisha mashabiki wa muziki kutoka pande mbili, wale wanaokubali zaidi kazi za Jambo Squad kutoka Kaskazini mwa Tanzania, na wale wa Linex ambaye muziki wake unawavutia watu wa rika mbalimbali ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.


Diamond: Nimelisoma soko la muziki

 
 Msanii Diamond Platinumz, amesema kuwa, kwa sasa baada ya mafanikio makuwa ya remix ya ngoma yake ya My Number One, picha linaendelea ambapo atawazawadia mashabiki wake kolabo nyingine kubwa ya kimataifa hivi karibuni.


Diamond amesema kuwa, harakati anazofanya sasa ni kufanya Tanzania na muziki wake ufike mbali zaidi, ambapo amefichua kuwa, amekuwa akipokea maombi mengi kutoka kwa wasanii wa nje kwa ajili ya kufanya kolabo nae, na hapa anaeleza juu ya mchongo huu, vile vile kolabo nyingine za kimataifa ambazo zitatoka baada ya My Number one Remix.
Msanii huyu amesema pia, baada ya kuusoma vizuri muziki barani Afrika, amegundua kuwa kuna soko kubwa la muziki wa Afrika Magharibi, na pia kuna soko la muziki wa Afrika kwa ujumla, na sasa atakua akitoa ngoma zake kwa kufuata ramani ya soko hili.
Diamond pia amewakata mashabiki wake kufahamu kuwa, hivi karibuni kuna kazi kubwa ambazo amefanya na Iyanya pamoja na D'banj ambao ni wasanii wakuba Nigeria, kazi ambazo zinatarajia kutikisa vilivyo pindi zitakapotoka.


Sunday, March 23, 2014

(Video Mpya) Shilole - CHUNABUZI (EXPLICIT)

Mambo 10 usiyoyajua kumhusu Wyre kutoka Kenya


 

Ameshinda tuzo nyingi sana kutokana na aina yake ya uimbaji, ambao ni Reggae na Dancehall. Pia umaarufu wake uliongezeka zaidi pale alipomshirikisha katika nyimbo yake mwanadada Alaine katika wimbo wake wa “Nakupenda Pia” Kama bado hujamjua namzungumzia Wyre kutoka kenya.
 
Pamoja na kua ni maarufu sana lakini ni mambo machache sana yanajulikana kuhusu maisha yake ukiachana na mziki. Akifanya mahojiano na Tovuti ya Niaje ya Kenya, Wyre aliamua kutaja mambo kumi hatuyajui kuhusu yeye
  1. Gari yake ya kwanza kumiliki ilikua Subaru impreza
  2. Anapendelea zaidi magari yanayotengenezwa na kampuni ya BMW
  3. Hatumii madawa au kilevi cha aina yeyote ile
  4. Mchumba wake wa kwanza alimpata akiwa darasa la 8.
  5. Mwanamke wa ndoto zake ni mke wake aliye nae sasa.
  6. Amesomea mass communication
  7. Mara yake ya kwanza kuperform stejini ni alipokua High School ambapo alifanya akapela akiwa na rafiki zake.
  8. Anasema bado anahitaji kujulikana zaidi.
  9. Kwenye upande wa mavazi anapenda nguo za Sean John
  10. Siku ambayo hatasahau ni siku aliyoshinda tuzo ya msanii chipukizi katika tuzo za International Reggea Awards.

MAPROFESSOR WA MUZIKI TANZANIA.


 

Katika historia ya muziki Tanzania kuna watu wa-3 tu waliopata kuitwa ma-professor. Mmoja kwenye muziki wa dansi (BONGO DANSI), mmoja Taarab na mwingine bongo flava.

Kwenye BONGO FLAVA kuna Professa Jay wa Mitulinga, Joseph Haule. Huyu jamaa ameanza kujulikana zaidi tokea enzi za Hard Blasters Crew (HBC) akiwa na Fanani na Willy. Watu wanakumbuka wimbo wa Chemsha Bongo” na “Mamsapu”.Kwenye TAARAB kuna mtu alikuwa anaitwa Professor Mohamed Mrisho. Huyu alipata kutunga wimbo wa
“Nyama ya Bata” alipokuwa na TOT Plus miaka ya mwanzoni mwa 1990. Wimbo huu ulikuwa katika album ya “TX MPENZI”, albamu ambayo pia ilikuwa na wimbo makini wa “Zumbukuku” uliotungwa na Ally Star.
Kwenye MUZIKI WA DANSI kulikuwa na Professor Omar Shaaban. Huyu alikuwa ni bingwa wa kupiga rhythm guitar Africa Mashariki na kati miaka ya 70 na 80. Huyu ni mmoja wa waanzilishi wa kundi la Simba Wanyika. Baadaye alikuwa ndio kiongozi wa maasi ya mwaka 1978 yaliyosababisha kundi kugawanyika na kuzaliwa Les Wanyika.

Kwenye picha huyu ndiye Professor Omar Shaaban ambaye ni mtunzi wa wimbo wa “Sina Makosa”, wimbo wa pili kwa umaarufu kuliko nyimbo zote zilizopata kutokea katika historia ya Afrika Mashariki.
Katika hawa maprofessor watatu, wawili wameshatangulia mbele za haki. Mmoja alizikwa Tanga, Tanzania. Mwingine alizikwa Nairobi, Kenya makaburi ya Langata.


[ Ngoma Mpya ] Akwera Ft Uhhh – Tikisa

tikisa6 


HARUSI YA KIMILA YA PETER OKOYE WA P SQUARE YAFANYIKA JANA NA KURUSHWA LIVE DSTV































Zikiwa zimepita siku chache tangu Peter Okoye mmoja wa wasanii mapacha wanaounda kundi la P-Square kufunga ndoa na mchumba wake wa siku nyingi. ..Jana (march 22) ilikuwa big day kwa star wa kundi la P-Square Paul Okoye na mpenzi wake wa miaka kumi Anita Isama, waliofanikisha harusi yao ya kimila iliyofanyika katika mji wa Port Harcourt, Nigeria na kuhudhuriwa na ma-star mbalimbali.

 unnamed
 Licha ya harusi hiyo kuhudhuriwa na watu wengi maarufu lakini pia ilioneshwa live na kituo cha runinga cha HIP TV ambacho kinaonekana kupitia DSTV.